Harmorapa amponda mzungu wa Harmonize
Harmorapa akiwa kwenye pozi.
Akizungumza kuhusu mpenzi huyo wa Harmonize, alifunguka kwamba: “Mimi namuona yule Mzungu wa Harmonize ni bibi tu, hajaopoa demu pale ila kaopoa mpenzi ambaye ni bibi. Yaani ni kama mimi niishi na bibi yangu, ndo Harmonize kama anaishi na bibi mzaa mama yake.”
Harmorapa alishawahi pia kufunguka mengi juu ya yeye kumpenda Wema aliposema yupo tayari kumlipia fedha yoyote ile kwa ajili ya kuishi naye. Lakini, baadaye aligeuka na kumponda mrembo huyo akidai ana umri mkubwa pia.
Mwanamuziki huyo machachari ‘alimshauri’ Harmonize atafute mpenzi anayeendana na umri wake.
Comments
Post a Comment