EXCLUSIVE UPDATES: Uchaguzi Mkuu Kenya Agosti 8, 2017

[​IMG]

[​IMG]

KENYA: Uchaguzi Mkuu unafanyika leo, Wapiga kura milioni 19 watachagua Rais, Wabunge, Maseneta, Magavana, Madiwani na Wawakilishi wa Wanawake.

Raia wa Kenya wataamua nani atakuwa Rais wao na Makamu wa Rais kwa miaka 5 ijayo.

Ushindani mkubwa sana uko kati ya vyama vya Jubilee na NASA na wagombea wake wa Urais, Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.

Pamoja na kura ya urais pia watapiga kura ya kuchagua magavana wa Kaunti, wawakilishi wa kata(madiwani) na wawakilishi wa Seneti na Bunge.

Fuatilia hapa kupata updates za uchaguzi huu unaohusisha takribani wapiga kura milioni 20 waliojiandikisha.

Waliojiandikisha: Milioni 19
Vituo vya kupigia kura: 40,000
Idadi ya Wakenya: Milioni 48

UPDATES:

tapatalk_1502149309045.jpeg
Vijana wa Kaunti ya Kisumu wakiwa kwenye mstari wakisubiri kupiga kura.

tapatalk_1502149347813.jpeg
Kaunti ya Siaya nao hawajataka kuwa nyuma.

[​IMG]
Man on a life support machine casts his vote at Dandora Primary School

[​IMG]
Voters patiently waiting to cast their votes at Moi Avenue primary, Starehe constituency in Nairobi

LIVE TEXT FEED:

08:50am updates

> Rais Uhuru Kenyatta amewataka wakenya wajitokeze kwa wingi kuchagua viongozi wanaowapenda

> NASA wameamua kufuta kauli yao dhidi ya KDF baada ya kuhakikishiwa kuwa kila kitu kitaenda kwa mujibu wa taratibu na sheria

> Waangalizi wa EU wameridhika na mwenendo unaoonekana hadi sasa

> Wakenya wengi wamekiri kuwepo kwa propaganda kwa njia ya mitandao ya kijamii na hivyo kuwachanganya wengi

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande

Kumbukumbu ya kuundwa kwa chama cha AA mwaka 1927 chini ya Sesilia Matola